ISSN 0865-6941 | Toleo Na. 307 | Machi 2016 | |
Njia nzuri ya kujikinga na RadiNa Prof. Kamazima Lwiza Profesa wa Fizikia ya Anga, New York, Marekani Mwanachama wa FOB na BUDEFO Mtaalamu wetu juu ya Fizikia ya Anga hapa anatujuza na huku akitutahadharisha kuhusu namna nzuri ya kuchukua tahadhari wakati hali ya hewa inapotubadilikia na kuwa ni mawingu, mvua na radi. Ni busara kwa wanafunzi na hata watu wengine kuyazingatia mawaidha haya ya kisayansi na ambayo kamwe hayazingatii mambo ya imani za watu juu ya RADI na mtikisiko wake. Pigo moja la radi linakadiriwa kuwa na Volt 125,000,000 za umeme. Kwa sasa hakuna njia kamili ya kujikinga na maafa ya radi isipokuwa kuna njia za kupunguza maafa kama ifuatavyo: Ukiwa ndani ya nyumba ukaanza kuona dalili za mvua ya radi usitoke nje. Wala usiharakishe kutoka nje baada ya dhoruba – subiri ipite nusu saa baada ya ngurumo ya mwisho. Vifo vingi vya radi hutokea dakika chache baada ya dhoruba kupita. Ukiwa nje ukaanza kuona dalili za mvua ya radi usingoje mvua ianze kunyesha – tafuta sehemu mahali hususani jengo lenye kuta na paa (k.m. nyumba, kanisa, msikiti, duka, n.k.). lakini siyo kioski, au veranda. Kama hakuna jengo ingia kwenye gari au basi lakini hakikisha hugusi sehemu yoyote yenye chuma. Usijikinge mvua chini ya mti au karibu na maji (ziwa au bwawa). Miti na maji hupitisha (conduct) umeme wa radi kwa urahisi. Sehemu nyingine za hatari ni nyika na viwanja vya michezo, kilele cha mlima, au mgongo wa mlima, mbele ya pango. Kama ukikumbwa na dhoruba na huna pa kukimbilia itabidi uchuchumae miguu yako ikutanishe pamoja (kwa sababu umeme wa radi huwa unaingilia mguu mmoja na kutokea kwenye mwingine – huongeza athari), na pia inamisha kichwa kwenye magoti. Kamwe usilale chini kwenye ardhi, kwa sababu radi ikiisha piga huwa inasambaa kupitia ardhini na kama umelala chini umeme utapita mwilini mwako. Ukiwa ndani ya nyumba usitumie simu ya waya – tumia ya mkononi. Usiguse mabomba ya jikoni wala bafuni. Chomoa TV (kuzima switch peke yake haitoshi na vifaa vingine kama air conditioner, kompyuta, n.k.). Kama una mwenzako akipigwa na radi, na huduma ya ambulance ipo wapigie simu mara moja, au tafuta njia nyingine ya kumfikisha hospitalini. Na unaweza kumshika anakuwa hana umeme ila ni vyema kumtafutia msaada wa kumpeleka hospitali haraka iwezekanavyo. Radi ikikukuta ziwani mambo sio mazuri. Ni vema kupiga makasia haraka sana kurudi ufukweni na kutafuta mahali pa kujikinga. Kama uko mbali na huwezi kufika pwani kama ni mtumbwi una sehemu ya kujisetiri ingia haraka bila hivyo kama ni ngalawa ya kawaida chuchumaa chini (usilale chini) na hakikisha hugusi maji. Kanuni ya thelathini – kwa – thelathini: Ukiona miali ya radi anza kuhesabu sekunde mpaka utakaposikia ngurumo. Muda ukiwa chini ya sekunde 30 basi ujue dhoruba iko karibu sana nawe. Ina maana huna muda wa kutafuta mahali pa kujisetiri – chuchumaa na kutanisha miguu yako. Hadithi za uongo – na – kweli (nyingi sio za kweli)
|
Mhariri Mkuu:Pd. Almachius Rwejuna
Cell:+255 784440 159 au +255 768 761 270
Mhariri Msaidizi: Gilbert J. Makwabe
Cell: +255 754 607 135
Mpiga Chapa:Mrs Judith Joseph
Cell: +255 755 788 690
Msambazaji:Sr Irene Ayebale
Cell: +255 782 172 797
|
Tunashughulika na Yafuatayo
|